Loading...
Propellerads

Walionunua SAMSUNG GALAXY Note 7 watakiwa kuzizima na kuzirudisha madukani

SAMSUNG GALAXY Note 7
Kampuni ya simu za mkononi ya SAMSUNG imetoa wito kwa watu wenye simu aina ya Galaxy Note SEVEN kuzizima mara moja wakati wakifanya uchunguzi kuhusu usalama wake.

Kampuni hiyo inataka kuchunguza kufahamu ni kwa nini simu hizo zinawaka moto.
Kampuni hiyo ya KOREA KUSINI imesema itasitisha uuzaji wa aina hiyo ya simu.
Kampuni ya SAMSUNG imesema watu walionunua jumla ya simu MILIONI MBILI na LAKI TANO, Septemba wazirejeshe madukani kutokana na malalamiko ya wateja kwamba betri za simu hizo zinalipuka.
Shuhuda wa tukio la kuwaka moto kwa simu hizo mwanamume mmoja wa jimbo la KENTUCKY, MAREKANI amesema aliamka na kukuta chumba kimejaa moshi uliotokana na simu mpya ya hiyo aliyoipata baada ya kurejesha ya zamani.
Shuhuda mwingine ni abiria kwenye ndege moja MAREKANI waliondolewa kwenye ndege kwa dharura baada ya simu ya GALAXY Note 7 kuanza kutoa moshi.
TANGAZO LA NDANI===
Facebook Blogger Plugin by SAMCHARDTZ

Chapisha Maoni

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright JUMBA LA HABARI | Designed By PRODUCER CHARD
Back To Top